Kuweka upya mandhari ya Kiafrika: Kijani na baridi

Fikiria kuweza kuwahamasisha na kuwawezesha mamiloni ya wakulima wadogo kurejesha ardhi zao kwa kutumia mbinu zilizo thibitika za usimamizi endelevu wa matumizi ya ardhi.

Je! Unaweza kufikiria athari kubwa ambayo itakuwa nayo katika upatikanaji wa mavuno ya mazao, mapato ya kaya, bioanuwai, upatikanaji wa maji, hali ya hewa ya maeneo husika  na mabadiliko ya hali ya hewa ulimwenguni? Na inaweza kufanyika, badala ya kusonga polepole kutoka eneo moja hadi lingine ardhini, kwa kuhamasisha kila mtu pamoja katika harakati moja iliyounganishwa, ya kimataifa?

Inayoleta pamoja mashirika yasiyo kiserikali , serikali, na makampuni ndiyo ambayo yameunganisha mkulima ndani ya Senegal na  mwingine ndani ya Malawi?

Ndani ya  Justdiggit, dhamira yetu ni kukijanisha Africa  ndani ya muongo mmoja ujao, na lengo letu ni kuhamasisha na kuwapa watu nguvu ulimwenguni kote kujiunga nasi.

Tanzania _ Justdiggit

TUNAPANUA WIGO WA KUONGOA MNADHARI YA ARDHI NDANI YA AFRIKA

Kazi zetu zinajumuisha kufungamanisha mbinu za kuongoa mandhari  ya ardhi na nguvu ya vyombo vya habari , mawasiliano, taarifa na tekonolojia ya simu. Juhudi zetu za kuongoa ardhi kwa kupitia mtandao mkubwa wa  vyombo vya habari  vya kimataifa kwa ajili ya kupanua wigo. Pia tunashirikiana na washirika wa ndani, kitaifa na kimataifa na wenye juhudi

KWANINI AFRIKA?

Afrika ina aina nyingi za mifumo ya ikolojia, mandhari, na viumbe hai. Ingawa maeneo mengi yanakabiliwa na changamoto za uharibifu wa ardhi, bara hili pia lina uwezo mkubwa zaidi wa urejeshaji wa mazingira duniani. Katika nchi na jamii zake nyingi, kuna fursa nyingi za kulinda na kufufua baadhi ya maeneo ya asili yenye thamani kubwa duniani. Ndiyo maana tunaelekeza juhudi zetu barani Afrika.

Kuwawezesha wakulima kupitia programu za kukijanisha

Katika program zetu zote za kurudisha mazingira tulizonazo, tunatafuta njia bora za kushirikiana kwa karibu na washirika na jamii. Faida dhahiri ya kijamii na kiuchumi kwao pia inatiwa moyo kwa kuhusishanisha  vitu hivo  ili tuweze kuhakikisha mipango hiyo ni endelevu.

decorative image

Mkulima akifanya mazoezi ya Upandaji miti huko Singida, Tanzania

KUANZISHA MAPINDUZI YA KIJANI

Tazama hadithi yetu

Ikiwa tunataka kuipooza  sayari kwa muongo mmoja, kila mtu anahitaji kuwa kwenye mabadiliko. Lengo letu ni kuhamasisha, kuunganisha na kuwezesha kizazi kizima, kukuza harakati za kurudisha mazingira.

poster