Miradi ya kukijanisha
Dodoma, Tanzania
Dodoma, Tanzania

Tuko kwenye dhamira ya kukijanisha Afrika na kuipooza dunia. Pamoja na mamilioni ya wakulima pamoja na wewe.
Tuko katika tatizo la mabadiliko ya hali ya hewa duniani. Sayari yetu inapata joto kwa haraka. Kwa bahati nzuri, kuna suluhisho: ikiwa tutarudisha hali ya asili kwa kutumia suluhu za asili zenye gharama nafuu, tunaweza kupunguza ongezeko la joto kwa asilimia 37! Hii itanufaisha hali ya asili, bioanuwai na watu kila sehemu, na itaisadia kuipooza sayari yetu.
Makinga maji kama tunavopenda kuyaita “Dunia inatabasamu” ni mashimo ya nusu duara yanayotumika kuvuna maji ya mvua.
Yamechimbwa katika miradi yetu katika Afrika ili kuvuna maji ya mvua ambayo yangeweza kupotea kwa kupita katika ardhi kavu isiyo na kitu. Kwa kuchimba makinga maji. Tunaweza kukijanisha eneo kubwa ndani ya muda mchache, kunufaisha bio anuwai, asili, wat una na matokeo yake hali ya hewa.
Ikiwa unataka kufanya mabadiliko ya ulimwengu, unahitaji kuwa kila mahali: habari, matangazo, vituo vya kijamii, mazungumzo, na zaidi ya yote katika mioyo na akili za watu. Ili kufanya hivyo, tunatumia nguvu ya vyombo vya habari na mawasiliano, kujenga utayari na uelewa na kuonyesha kuwa kwa pamoja tunaweza kuwa na athari chanya na muhimu kwa mabadiliko ya hali ya hewa.
Kampeni zetu za kimataifa za uelimishaji mtandaoni na nje ya mtandao zinatengenezwa ili kukuza njia za asili na kuhamasisha, kuunganisha na kuamsha kizazi kizima na kukuza harakati za kurudisha mazingira.
Ndani ya benki zetu za mbegu za nyasi, wanawake wa Kimasai hukua, huvuna, na kuuza nyasi (nyasi) na mbegu. Wanapata mapato kwa kuuza kwenye masoko ya ndani au kwa mashirika. Hifadhi za mbegu za nyasi huunda eneo lenye kijani katika ardhi kame, na nyasi ambayo wanawake huvuna ni chakula cha mifugo yao wakati wa kiangazi.
Kwa jumla tuna benki 12 za mbegu za nyasi huko Kuku na OOGR, Kenya.
Tunazingatia ambapo tunaweza kupata athari Zaidi: Afrika. Njia yetu ni kuwamasisha na kuwawezesha mamilioni ya ya wakulima wadogo kukijanisha ardhi yao. Athari kubwa ya kukijanisha Afrika itanufaisha hali ya asili, bioanuwai na watu kila sehemu na kusaidia kuipooza dunia.
Tunaungwa mkono na mtandao wa ulimwengu wa chapa na mashirika ambayo hutusaidia katika dhamira yetu ya kutuliza sayari.
Washirika wote